Umoja wa Mataifa wamtambua Ouattara.
9 Desemba 2010Matangazo
Aidha baraza hilo pia limetoa wito wa pande zote kuheshimu ushindi alioupata kiongozi wa upinzani nchini humo Alassane Ouattara, kufuatia uchaguzi wa rais uliofanyika nchini humo mwezi uliopita.
Katika taarifa iliyosomwa na balozi Brooke Anderrson, ambaye nchi yake kwa sasa ndiyo inashikilia nafasi ya Urais, baraza hilo limesema linalaani juhudi zozote zitakazovuruga matakwa ya watu ama kuhujumu uaminifu wa zoezi hilo la uchaguzi.
Rais aliyemaliza muda wake Laurent Gbagbo amekuwa akikataa mpaka sasa kukabidhi madaraka kwa mpinzani wake Alassane Ouattara, ambaye ameshinda katika uchaguzi huo wa Rais.
Urusi imekuwa ikikawiza jaribio la baraza hilo la usalama kumlazimisha Bwana Gbagbo kuondoka madarakani.