Wanamichezo mashuhuri wa Ukraine waliojiunga na vita
Wladimir Klitschko (Bondia)
Wladimir Klitschko ni ndugu wa Vitali ambaye alishinda medali ya dhahabu katika Olimpiki ya 1996 kabla ya kutwaa ubingwa wa IBO, WBA, IBF na WBO katika uzito wa juu. Alistaafu mwaka 2016, lakini mwanamasumbwi huyo mwenye miaka 45 amejiunga na jeshi la akiba la Ukraine kwa ajili ya kupambana katika vita dhidi ya Urusi, kama ilivyo kwa kaka yake, Vitali.