1. Inhalt
  2. Navigation
  3. Weitere Inhalte
  4. Metanavigation
  5. Suche
  6. Choose from 30 Languages
Matangazo
Matangazo
Matangazo
HABARI

Habari za Ulimwengu | 11.01.2022 | 14:00

Wabunge wa Kazakhstan wachagua waziri mkuu mpya

Wabunge nchini Kazakhstan wamepiga kura leo na kumuidhinisha Alikhan Smailov kuwa waziri mkuu mpya katika wakati taifa hilo la Asia ya kati linajaribu kurejesha utulivu baada ya siku kadhaa za machafuko. Smailov mwanasiasa anayeungwa mkono na rais Kassym-Jomart Tokayev wa Kazakhstan tayari alikuwa anashikilia wadhifa huo kwa muda, baada ya kuvunjwa kwa serikali ya zamani wiki iliyopita. Kuidhinishwa kwake kumefanyika saa chache baada ya rais Tokayev kutangaza kurejea kwa utulivu kamili nchini humo baada ya vurugu za wiki iliyopita zilizosababisha vifo vya watu 160 na maelfu wengine kukamatwa. Katika hatua nyingine rais Tokayev ametangaza leo kuwa ujumbe wa kijeshi ulioongozwa na vikosi vya Urusi uliotumwa nchini humo kutuliza ghasia umekamilisha kazi yake na utaanza kuondoka ndani ya siku mbili zinazokuja.

Salamu za rambirambi zatumwa kufuatia kifo cha rais wa Bunge la Ulaya

Viongozi kadhaa barani Ulaya leo wametuma salamu za rambirambi kufuatia kifo cha rais wa bunge la Umoja wa Ulaya David Sassoli aliyeaga dunia katika hospitali moja nchini Italia alikolazwa kwa matibabu. Rais wa Halmashauri Kuu ya Umoja wa Ulaya Ursula vod der Leyen amesema Ulaya imepoteza mtu muhimu aliyejitolea kupigania misingi ya demokrasia na ustawi wa Umoja wa Ulaya. Waziri Mkuu wa Italia Mario Draghi amemtaja Sassoli kama alama ya utu na ukarimu sifa ambazo zinafahamika na wanasiasa wenzake aliofanya nao kazi kwenye mataifa mengi barani Ulaya. Sassoli, aliyechaguliwa kuwa rais wa Bunge la Ulaya mwaka 2019 amefariki dunia mapema leo baada ya kulazwa hospitali tangu Disemba 26 kutokana na matatizo makubwa ya mfumo wa kinga ya mwili.

WHO: Nusu ya watu barani Ulaya wataambukizwa kirusi cha Omicron

Shirika la Afya la Umoja wa Mataifa limesema zaidi ya nusu ya watu wote barani Ulaya wanatazamiwa kuwa wataambukizwa kirusi cha corona aina ya Omicron katika muda wa miezi miwili inayokuja. Mkuu wa WHO kanda ya Ulaya Hans Kluge amesema tathmini hiyo ni kwa mujibu wa taasisi ya takwimu za afya ya IHME na imetolewa wakati kirusi cha omicron kinaendelea kusambaa kwa kasi duniani. Bara la Ulaya limekuwa kitovu cha idadi kubwa ya maambukizi ya virusi vya corona hali iliyopelekea serikali nyingi kutangaza vizuizi vipya na kutanua kampeni ya utoaji chanjo za nyongeza dhidi ya Covid-19. WHO imesema ingawa kirusi cha omicron kinasambaa haraka ikilinganishwa na aina nyingine zilizotangulia, chanjo zilizoidhinishwa bado zinaweza kutoa kinga dhidi ya watu kupata maradhi makali na hata kifo.

Serikali ya Mali yaitisha maandamano kulaani vikwazo vya ECOWAS

Watawala wa kijeshi nchini Mali leo wametoa mwito wa kufanyika maandamano ya nchi nzima siku ya Ijumaa kupinga mkururo wa vikwazo vikali ilivyowekewa nchi hiyo na Jumuiya ya Kiuchumi ya nchi za Afrika magharibi, ECOWAS kwa sababu ya kuchelewesha uchaguzi. Serikali hiyo ya mpito imesema vikwazo vilivyowekwa ikiwemo kufungwa kwa mipaka na vizuizi vya kibiashara ni vikali na kwa hivyo umma wa Mali ni lazima ujitokeze kulaani uamuzi huo wa Jumuiya ya ECOWAS. Hayo yanajiri wakati kiongozi wa mapinduzi nchini Mali kanali Assimi Goita amewarai viongozi wa mataifa ya Afrika Magharibi kutafakari upya vikwazo hivyo ambavyo vimeanza kutekelezwa jana. Goita amesema yuko tayari kwa mazungumzo na jumuiya ya ECOWAS ambayo inaiadhibu nchi yake kwa kukataa kuandaa uchaguzi wa kidemokrasia mwezi Februari kama ilivyokubaliwa hapo awali.

Rais wa Ukraine ataka kuitishwa kwa mkutano wa kimataifa kumaliza vita nchini Ukraine

Rais wa Ukraine Volodymyr Zelensky leo ametoa mwito wa kufanyika kwa mkutano mwingine wa kilele pamoja na Ufaransa, Ujerumani na Urusi ili kutatua mzozo wa mapigano mashariki mwa Ukraine. Taarifa iliyotolewa baada ya Zelensky kufanya mazungumzo na wanadiplomasia wa Ulaya, imesema kiongozi huyo amesisitiza umuhimu wa kutafuta suluhisho la kudumu la mzozo nchini Ukraine na kwamba yuko tayari kuchukua maamuzi yanayohitajika. Zelensky alikutana kwa mara ya kwanza na rais Vladimir Putin wa Urusi mwaka 2019 wakati wa mazungumzo ya amani mjini Paris yaliyoitishwa na viongozi wa Ufarana na Ujerumani. Hata hivyo mazungumzo hayo ya awali hayakufanikiwa kumaliza mzozo kati ya vikosi vya Ukraine na wapiganaji wanaoungwa mkono na Urusi yaliyozuka mwaka 2014.

Vikosi vya serikali ya Yemen vyalikamata jimbo la Shabwa kutoka kwa waasi

Vikosi vya serikali inayotambuliwa kimataifa nchini Yemen leo vimerejesha udhibiti kamili wa jimbo la kusini la Shabwa kutoka mikononi mwa waasi wa Houthi wanaungwa mkono na Iran. Maafisa wa serikali ya Yemen wamesema wapiganaji wake wakisaidiwa na mashambulizi ya anga kutoka muungano wa kijeshi unaoongozwa na Saudi Arabia wamefanikiwa kulikamaa jimbo hilo baada ya siku 10 za mapigano makali. Gavana Awad al-Awlaki ametangaza "kukombolewa kwa jimbo Shabwa" na kuzishukuru Saudi Arabia na Umoja wa Falme za Kiarabu zinazofadhili muungano wa kijeshi unaopambana dhidi ya waasi wa Houthi. Kukamatwa kwa jimbo la Shabwa kutaviwezesha vikosi vya serikali kukata njia zote za muhimu zinazotumiwa na waasi wa Houthi katika kampeni yake ya kijeshi ya kulidhibiti jimbo la Marib ambalo ni ngome ya mwisho ya serikali kaskazini mwa Yemen

Waziri Mkuu wa Uingereza aandamwa na kashfa nyingine ya kufanya sherehe wakati wa vizuizi vya Covid-19

Waziri Mkuu wa Uingereza Boris Johnson anakabiliwa na kashfa nyingine kubwa kuhusiana na madai kwamba serikali yake ilikiuka vizuizi vikali vya kukabiliana na janga la virusi vya corona kwa kufanya shughuli zilizopigwa marufuku. Katika madai ya hivi karibuni kabisa, Johnson na wenzake kadha wanatuhumiwa kufanya dhifa ya zaidi ya watu 100 kwenye makaazi rasmi ya kiongozi huyo mnamo Mei 2020 wakati ambao sherehe kama hizo zilikuwa zimezuiwa kisheria. Barua pepe ilivuja jana Jumatatu inaonesha afisa mmoja katika ofisi ya waziri mkuu iliyoko mtaa wa Downing, mjini London aliwaalika watumishi wengine zaidi ya 100 katika hafla iliyohudhuriwa na Johnson mwenyewe na mkewe Carrie. Ufichuzi huo ambao yumkini utakuwa na taathira kubwa kwa kiongozi huyo, unafuatia madai mengine kama hayo yaliyotolewa mwezi uliopita kwamba ofisi yake ilifanya sherehe kadhaa kuelekea sikukuu ya krismasi mwaka 2020, licha ya kwamba mikusanyo ilikuwa imepigwa marufuku.

MATUKIO YA KISIASA
MATUKIO YA AFRIKA
MASUALA YA JAMII
MICHEZO
HABARI KWA LUGHA YA KIINGEREZA

Matangazo
Tazama vidio 03:47

Vidio zaidi

Utawala Bora na uwajibikaji wa viongozi

Utawala Bora na uwajibikaji wa viongozi

Tansania Präsidentin Samia Suluhu Hassan

Kabudi na Lukuvi wapangiwa kazi maalum

Symbolbild I Gebiss I Dentalmedizin

Kurunzi Afya: Usafi wa kinywa na meno

Msichana Jasiri

Msichana Jasiri

Kenya: Kilimo cha maji kinachozingatia mazingira

Kenya: Kilimo cha maji kinachozingatia mazingira

TUFUATILIE KATIKA MITANDAO YETU YA KIJAMII