PARIS.Baraza jipya la mawaziri latangazwa nchini Ufaransa
18 Mei 2007Matangazo
Rais Nicolas Sarkozy wa Ufaransa ametangaza baraza la mawaziri ambapo nusu ya nyadhifa zitashikwa na wanawake.Waziri mpya wa mambo ya nje atakuwa bwana Bernard Kouchner , msoshalisti , alieanzisha shirika la madaktari wasiokuwa na mipaka.
Baraza hilo jipya chini ya waziri mkuu Francois Fillon lina mawaziri 15 .