OSLO: Muhammad Yunus kutoka Bangladesh atunukiwa tuzo la amani la Nobel 2006
13 Oktoba 2006Matangazo
Tuzo la amani la Nobel mwaka wa 2006 limekabidhiwa raia wa Bangladesh Muhammad Yunus na Benki yake Grameen Bank aliyeunda kuwasaidia watu maskini. Imetangaza muda mfupi tu uliopita kamati ya Nobel mjini Oslo nchini Norway. Mwaka jana nishani hiyo ya Nobel ilikabidhiwa Shirika la kimataifa la nguvu za atomiki na mkurugenzi wake mkuu Mohammed El Baradei.
Haikutarajiwa kuwa Muhammad Yunus ndie angeibuka na tuzo hilo la amani la Nobel.