Mgomo wa reli wakaribia kumalizika Ufaransa
22 Novemba 2007Matangazo
Mgomo wa reli uliokwamisha huduma za usafiri nchini Ufaransa tangu siku tisa zilizopita, unakaribia kumalizika.Madereva wengi wa treni walianza kurejea kazini baada ya majadiliano ya upatanisho kuanza mjini Paris.
Mgomo huo uliochochewa na mipango ya serikali kutaka kufanya mageuzi katika mfumo wa malipo ya uzeeni ya wafanyakazi wa mashirika ya reli, umesababisha hasara ya kama Euro milioni 400 kila siku moja.