KUWAIT Mwanamke wa kwanza ateuliwa kuwa waziri
13 Juni 2005Matangazo
Waziri mkuu wa Kuwait, Sheikh Sabah al-Ahmad al-Sabah, amemteua waziri wa kwanza mwanamke katika baraza lake la mawaziri. Shirika la habari la taifa limeripoti kwamba waziri mkuu huyo amemteua Massouma Mubarak kuwa waziri wa mipango na maswala ya maendeleo. Uteuzi huo umefanywa majuma machache baada ya Kuwait kuwapa wanawake haki ya kupiga kura.