1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Iran yasema "haina imani" na Marekani kwenye mazungumzo

15 Mei 2026

Iran imesema leo Ijumaa kuwa haina imani na Marekani linapohusika suala la mazungumzo ya kumaliza vita lakini imesisitiza kwamba iko tayari kwa majadiliano pale Washington itakapoonesha dhamira ya dhati.

https://p.dw.com/p/5Dops
Mkutano wa mawaziri wa BRICS- 2026 | Waziri wa Mambo ya Kigeni wa Iran Abbas Araghchi New-Delhi
Waziri wa Mambo ya Kigeni wa Iran Abbas Araghchi akishiriki mkutano wa mawaziri wa kundi la BRICS nchini India. Picha: Adnan Abidi/REUTERS

Hayo yameelezwa na Waziri wa Mambo ya Kigeni wa Iran Abbas Araghchi pembezoni mwa mkutano wa mawaziri wa mataifa yanayounda kundi la BRICS unaofanyika kwenye mji mkuu wa India, New Delhi.

Ama kuhusu suala la kufungwa kwa Ujia wa Bahari wa Hormuz mwanadiplomasia huyo wa Iran, amesema, "Kwa tunavyofahamu, Mlango Bahari wa Hormuz uko wazi, na meli zote zinapita isipokuwa meli zinazomilikiwa na nchi zilizo kwenye vita na sisi, zile zinazopigana nasi"

Marekani na Iran zilitangaza kusitisha vita kwa muda mwezi uliopita lakini hadi sasa zimeshindwa kufikia makubaliano ya kudumu ya amani licha ya juhudi nzito za kidiplomasia zinazoongozwa na Pakistan.