1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Urusi yahimiza uvumilivu mzozo wa Iran na Marekani

29 Januari 2026

Urusi imeziomba Marekani na Iran kuvumiliana na kukaa kwenye meza ya mazungumzo kumaliza mvutano badala ya vita, katika wakati Marekani imetangaza kutoondowa uwezekano wa kuishambulia Iran

https://p.dw.com/p/57hls
Rais Vladimir Putin Urusi
Rais Vladimir Putin UrusiPicha: Alexei Danichev/Reuters

Urusi imesema hivi leo kwamba bado kuna nafasi ya mazungumzo kutatuwa mvutano kati ya mshirika wake Iran na Marekani baada ya rais Donald Trump kutishia kuishambulia Jamhuri hiyo ya kiislamu.

Mgogoro wa Mashariki ya Kati

Msemaji wa Ikulu ya Urusi, Dmitry Peskov amewaambia waandishi habari kwamba kuna uwezekano wa wazi wa kufanyika mashauriano kati ya pande hizo mbili na kutowa mwito wa kuvumiliana.

Wasiwasi wa kitisho cha Marekani kuishambulia Iran

Urusi pia imesema iko tayari kuondowa wafanyakazi wake katika kituo cha Nyuklia cha Buscher nchini Iran ikihitajika. Kwa upande mwingine Uturuki ambayo imetangaza kujiandaa kuimarisha usalama kwenye mpaka wake ikiwa mzozo huo utaongezeka, imejitolea kuwa msuluhishi kati ya Washington na Tehran.

Waziri wa mambo ya nje wa Iran Abbas Aragchi ambaye anaitembelea Ankara kesho Ijumaa amesema vikosi vya nchi yake viko tayari kujibu mashambulio ikiwa Marekani itashambulia.