Rais Donald Trump amesema anajutia uamuzi wa kumteua Jeff Sessions kuwa waziri wa sheria. Mzozo kati ya Ujerumani na Uturuki umezidi makali baada ya kukamatwa kwa watetezi 6 wa haki za binadamu nchini Uturuki.Kenya imeamuru wauzaji wote wa chakula nchini humo kupimwa afya, baada ya kipindupindu kuuwa watu wanne Nairobi. Na bangi imeanza kuuzwa rasmi katika maduka ya dawa nchini Uruguay.