1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

ROME:Bunge laridhia fedha zaidi kwa jeshi la Italia nchini Afghanistan

28 Machi 2007
https://p.dw.com/p/CCEz

ROMA

Waziri Mkuu wa Italia, Romano Prodi amefanikiwa kupata kura za kutosha bungeni zinazomruhusu kupata fedha za ziada kwa ajili ya majeshi ya nchi hiyo huko Afghanistan.

Mwezi uliyopita suala hilo liliibua mzozo serikalini, wakati Waziri Mkuu huyo wa Italia alipopigiwa kura ya kutokuwa na imani naye.

Waziri wa Mambo ya Nje wa Italia Massimo D´ Alema amepongeza hatua hiyo akisema kuwa kushindwa kupitishwa kwa muswaada huo wa kuongeza fedha kwa kikosi cha askari elfu mbili wa Italia katika jeshi la NATO ingekuwa aibu.