Mwanajeshi wa Vita Vikuu vya Pili vya Dunia azungumza
1 Septemba 2009Matangazo
Hiyo ndio ilikuwa operesheni ya kwanza ya kijeshi katika Vita Vikuu vya Pili vya Dunia. Wakati huo huo, vikosi 62 vya jeshi la Ujerumani, vikisaidiwa na ndege 1,300, vilianza kuivamia Poland. Vita hivyo vilitapakaa katika sehemu mbali mbali za dunia, na medani za vita pia zilitanda huko Afrika na Asia, ambako washirika wa Ujerumani -Wajapani na Wataliana- walipambana pia na majeshi ya Waafrika kutoka makoloni ya Muengereza, kama vile yale ya Afrika Mashariki. Mmoja aliyeshiriki katika vita Vikuu vya Pili vya Dunia ni Ali Sykes kutoka Tanganyika ambaye alipelekwa Burma kuyasaidia majeshi ya Kiengereza yaliokuwa yanapambana na Wajapani. Othman Miraji Na Bw Ali Sykes.
Mahojiano/Othman Miraji/Ali Sykes