Libya-Baraza la Usalama
27 Februari 2011Baraza la Usalama la Umoja wa mataifa limepitisha kwa sauti moja hatua dhidi ya kiongozi wa Libya Muammar Gaddafi na jamaa zake.Vikwazo hivyo vinaanzia marufiku ya silaha,kusafiri na kufungwa akaunti zao.Taasisi hiyo muhimu ya Umoja wa Mataifa imefungua njia pia ya kuweza kuandamwa pengine Gaddafi na jamaa zake mbele ya Mahakama ya Kimataifa ya Uhalifu mjini The Hague kutokana na matumizi ya nguvu dhidi ya waandamanaji wanaoipinga serikali nchini Libya.Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa linaituhumu serikali ya mjini Tripoli kukiuka haki za binaadam.Katika maeneo yaliyokombolewa ya Libya,upande wa upinzani unaanza kujiandaa. Waziri wa zamani wa sheria Mustafa Abdul Ashleyl ametangaza kuundwa serikali ya mpito ambayo wanachama wake watatokea katika maeneo yote ya nchi hiyo.Benghazi ndio yatakayokua makao makuu ya serikali hiyo ya mpito-hadi Tripoli utakapokombolewa anasema waziri huyo wa zamani wa serikali ya Gaddafi.Kituo cha televisheni cha Al Djazira kimeripoti kwamba vikosi tiifu kwa Gaddafi vinaendelea kudhibiti sehemu kubwa ya Tripoli.