1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

BAGDAD:Desemba mwezi mbya kabisa kwa vikosi vya Marekani Iraq

31 Desemba 2006
https://p.dw.com/p/CCel

Jeshi la Marekani nchini Iraq limearifu kuuwawa kwa wanajeshi wake sita ndani na nje ya mji wa Baghdad na kuifanya idadi ya waliouwawa mwezi huu wa Desemba kufikia 109.

Idadi hiyo imepita ile ya mwezi wa Novemba.

Kwa jumla wanajeshi 2998 wa Marekani wameuwawa nchini Iraq tangu walipovamia mwaka 2003.Rais Gorge Bush anatarajiwa kutangaza mkakati wake mpya juu ya Iraq mwaka ujao unaoanza kesho.