Janga
Watu watatu wauawa baada ya Urusi kushambulia mji wa Odesa
6 Aprili 2026
Matangazo
Kampuni kubwa kabisa ya kibinafsi ya nishati nchini Ukraine, DTEK, imesema zaidi ya watu 16,000 wameachwa bila umeme kufuatia shambulizi hilo.
Moscow imekuwa ikiishambulia Ukraine masaa ya usiku ndani ya miaka yake minne tangu ilipoanza uvamizi wake wa kijeshi dhidi ya jirani yake na kuanzisha mgogoro mkubwa barani Ulaya ambao haujawahi kushuhudiwa tangu kumalizika kwa vita vya pili vya dunia.
Rais wa Ukraine Volodymyr Zelensky ametoa salamu zake za pole kwa familia za waliouwawa huku akiongeza kuwawatu wengine 16 wamejeruhiwa vibaya katika shambulizi hilo.
Zelensky ameongeza kuwa Urusi ilirusha droni zaidi ya 140 zilizoharibu pia maeneo yake ya nishati ya miji ya Chernihiv, Sumy, Kharkiv, na Dnipro.