Viongozi wa Ulaya walaani vikali tangazo la ushuru la Trump
18 Januari 2026
Mataifa ya Denmark, Norway, Sweden, Finland, Ufaransa, Ujerumani, Uholanzi na Uingereza yameonya kuwa vitisho hivyo vya ushuru vinakwamisha ushirikiano kati ya Ulaya na Marekani.
Awali, Trump alitangaza kuziwekea ushuru wa asilimia 10 nchi hizo zinazopinga juhudi zake za kukinunua kisiwa cha Greenland. Amesema ushuru huo utaendelea hadi mpango wa kuinunua Greenland utakapofanikiwa na huenda ukatekelezwa mpaka Juni 25 kama hakutafikiwa makubaliano.
Viongozi wa Ulaya wasema kitisho cha ushuru ni kosa kubwa
Kabla ya kauli hiyo ya pamoja Waziri Mkuu wa Italia mwenye uhusiano mzuri na Trump aliiionya hatua hiyo ya Trump aliyoitaja kuwa kosa kubwa. Naye msaidizi wa Kansela wa Ujerumani ambaye pia ni Waziri wa fedha Lars Klingbeil amesema Ujerumani na washirika wake wa Ulaya hawatakubali kushurutiswa na Marekani.