Trump azungumza na Merz, Takaichi baada ya kuondoka China
15 Mei 2026
Matangazo
Trump kwanza alizungumza na Kansela Friedrich Merz wa Ujerumani na kwa pamoja wamesisitiza msimamo wao wa kutaka kuizuia Iran kumiliki silaha za nyuklia na haja ya kufunguliwa kikamilifu kwa Mlango Bahari wa Hormuz.
Mazungumzo mengine ameyafanya na Waziri Mkuu wa Japan Sanae Takaichi yaliyojikita juu ya masuala kuhusu China hasa baada ya ziara ya siku tatu ya Trump mjini Beijing alikokutana na Rais Xi Jinpinga.
Mbali ya mazungumzo hayo, Trump amewaambia waandishi habari akiwa kwenye ndege ya Air Force One kuwa ziara yake ya China imefanikisha" kutiwa saini mikataba mizuri ya biashara" na "kutatua changamoto nyingi baina ya pande hizo mbili"