1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Chama tawala Georgia chaishtumu Marekani kwa kutumia vitisho

25 Mei 2024

Chama tawala nchini Georgia kimeisthumu Marekani kwa kutumia vitisho dhidi ya Georgia, kuhusiana na uamuzi wake wa kuwaweka vikwazo wabunge wanaounga muswada wa sheria kuhusu "mawakala wa kigeni."

https://p.dw.com/p/4gGs7
Georgia Tbilis | Kikao cha bunge | Maandamano
Picha hii iliyochukuliwa kutoka video, iliyotolewa na kituo cha televisheni cha Mtavari mnamo Jumanne, Mei 14, 2024, inaonyesha wabunge wa Georgia wakipigana wakati wa kikao cha bunge huko Tbilisi.Picha: Mtavari Channel/AP/picture alliance

Rasimu ya sheria  hiyo imesababisha mzozo wa kisiasa katika taifa hilo la kaukasusi ya kusini, ambapo waandamanaji wameingia mitaani katika baadhi ya maandamano makubwa zaidi tangu Georgia ilipopata uhuru wake kutoka iliyokuwa Jamhuri ya Kisovieti, kupinga muswada huo, ambao umelaaniwa pia na wakosoaji wa ndani, Marekani na Umoja wa Ulaya kuwa wa kiimla na ulioshawishiwa na Urusi.

Soma pia: Maandamano yanayopinga kubanwa kwa uhuru wa habari Georgia

Waziri wa mambo ya nje wa Marekani Antony Blinken alisema siku ya Alhamisi kuwa Marekani inaweka vikwazo vipya vya viza dhidi ya Georgia na kuanzisha mchakato wa kupitia upya ushirikiano kati ya mataifa hayo mawili kuhusiana na muswada huo, ambao utayataka mashirika yanayopokea zaidi ya asilimia 20 ya ufhadhili wake kutoka nje kujisali kama "mawakala wa kigeni."