Wajumbe wa Marekani na Iran wafanya mazungumzo
11 Aprili 2026
Waziri Mkuu wa Pakistan Shehbaz Sharif amesema anatumai Mazungumzo hayo yatasababisha kupatikana Amani ya kudumu.
Ujumbe wa Marekani unaaoongozwa na Makamu wa Rais wa Marekani unaokutana na Iran ni kwa ajili ya kufungua njia ya kudumu ya kukomesha mapigano. Ni mkutano wa Kwanza tangu vita vilipoanza.
Makubaliano ya kusitisha mapigano yaliosimamiwa na Pakistan yanatarajiwa kukabiliwa na vikwazo katika mazungumzo yanayoanza Jumamosi, Iran imeweka masharti kabla ya mazungumzo kuanza wakati ambapo Jeshi la Israel na wanamgambo wa Hisbollah wakiendelea kupigana kando ya mpaka wa kusini mwa Libanon.
Mapema siku ya Jumamosi Ujumbe wa Iran ulikutana na Waziri Mkuu wa Pakistan Shehbaz Sharif mjini Islamabad kabla ya kuanza mazungumzo na Marekani kuhusu kuvimaliza vita katika eneo the Mashariki ya Kati.
Serikali ya Iran imethibitisha kufanyika mkutano huo na imeongeza kusema kwamba maafikiano yote kati ya Iran na Marekani yatabainishwa mwishoni mwa mwa mwa mwa mkutano huo.
Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran Abbas Araghchi. Amesema nchi yake imeingia kwenye mazungumzo hayo lakini haina imani na Marekani kutokana na ugeugeu wake
Kwa upande wake makamu wa Rais wa Marekani JD Vance amesema iwapo Iran itakuwa na nia njema kwenye mazungumzo hayo basi Marekani nayo itafungua mikono yake.
Wakati huo huo chanzo kimoja kikuu kutoka Iran kimeliambia shirika the habari la Reuters kwamba Marekani sekubali kuziachilia mali zilizofungiwa za Iran zilizokuwa zimeshikiliwa Qatar na kwenye benki zingine za kigeni. Chanzo Hicho Kimesema Iran imekaribisha hat Hallo, Marekani. Hata hivyo Marekani imekanusha tetesi hizo.
Waziri wa Mambo ya Nje wa Pakistan Ishaq Dar, Ametoa mwito kwa Marekani na Iran kushiriki wa njia ya ya kujenga katika mazungumzo mazungumzo ya Islamabad.