MOSCOW: Russia na Belarusia zaafikiana kuhusu usambazaji wa mafuta.
13 Januari 2007Matangazo
Russia na Belarusia zimetia saini mkataba rasmi unaotanzua mzozo wa usambazaji wa mafuta ambao ulisababisha kukatizwa kwa huduma za mafuta kupitia bomba moja kuu kuelekea mataifa ya Ulaya.
Duru za habari zimemnukuu Waziri Mkuu wa Russia, Mikhail Fradkov, akisema tofauti zilizokuwepo zimetatuliwa.
Mkataba huo unajumuisha taratibu kadha za biashara ya mafuta ambayo Russia ilikuwa imedai kuwa Belarusia ilikuwa ikijipatia kwa njia ya udanganyifu.
Mzozo huo siku ya jumatatu iliyopita ulisababisha kufungwa kwa siku tatu bomba la kupitishia mafuta kuelekea mataifa ya Ulaya.