1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Kansela Merz alihutubia bunge mjini Berlin

29 Januari 2026

Kiongozi huyo wa Ujerumani amewatia shime viongozi wenzake wa Ulaya kuwa na umoja na kusimama kama kundi la kujitegemea mbele ya ulimwengu wenye utaratibu mpya

https://p.dw.com/p/57hlh
Kansela  Friedrich Merz akilihutubia bunge mjini Berlin.
Kansela Friedrich Merz akilihutubia bunge mjini Berlin.Picha: Liesa Johannssen/REUTERS

Kansela wa Ujerumani Fredrich Merz, amewataka viongozi wenzake barani Ulaya kushikamana na kujiweka kama kundi huru katika ulimwengu wenye utaratibu mpya unaozidi kuhodhiwa na Marekani, China na mataifa mengine yenye nguvu.

Katika hotuba yake mbele ya bunge mjini Berlin,kuhusu sera za nje za Ujerumani kiongozi huyo wa nchi, amesema Ulaya ni mbadala wa mitizamo ya kiimla na sera za kutumia mkono wa chuma duniani.

Merz asema Ujerumani haitojiunga sasa na Bodi ya Amani

Mtizamo wa Merz umetolewa wiki moja baada ya rais Donald Trump kulegeza msimamo kuhusu dhamira yake ya kukitwaa kisiwa cha Greenland.