1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
Migogoro

Marekani yaikosoa NATO kwa kuitenga katika mzozo wa Iran

9 Aprili 2026

Rais wa Marekani Donald Trump ameikosoa Jumuiya ya Kujihami ya NATO kwa kushindwa kuisaidia nchi yake katika mgogoro na Iran. Amezituhumu baadhi ya nchi kwa kuinyima Marekani fusa ya kutumia anga zao.

https://p.dw.com/p/5BuXC
Trump imeikosoa vikali Jumuiya ya Kujihami ya NATO kwa kushindwa kuipa ushirikiano kwenye vita vya Iran
Rais wa Marekani Donald TrumpPicha: Chip Somodevilla/Getty Images

Donald Trump pia amezikosoa nchi wanachama wa NATO kwa kwa kukataa kutoa msaada wa kijeshi katika suala la Mlango Bahari wa Hormuz. Ameyatoa malalamiko hayo mbele ya Katibu Mkuu wa Jumuiya hiyo Mark Rutte walipofanya mazungumzo Jumatano kwenye Ikulu ya Marekani, White House.

Mkuu wa NATO akiri baadhi ya nchi zilishindwa kutimiza wajibu

Aidha Katibu Mkuu Rutte amejibu kuwa anatambua kuwa badhi ya mataifa yalishindwa kutimiza wajibu wao lakini washirika hao wamekuwa wakisaidia na kuhakikisha kuwa wanatimiza ahadi zao.

Mgogoro ndani ya NATO kati ya Marekani na Washirika wa Ulaya umezidisha wasiwasi ndani ya Jumuiya hiyo huku wachambuzi wakionya kuwa uko mashakani kusambaratika