1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
Migogoro

Nchi za Kiarabu kujadili mashambulizi ya Iran Jumapili

7 Machi 2026

Jumuiya ya Mataifa ya Kiarabu (Arab League) imeitisha mkutano wa dharura utakaofanyika Jumapili 04.07.2026 ili kuyajadili mashambulizi yanayofanywa kutoka Iran kuelekea kwa baadhi ya nchi hizo hasa katika eneo la Ghuba.

https://p.dw.com/p/59z8L
Jumuiya ya nchi za Kiarabu imeitisha mkutano wa dharura kujadili mashambulizi ya Iran
Baadhi ya bendera za mataifa ya Jumuiya ya nchi za KiarabuPicha: Youssef Badawi/EPA/picture alliance

Katibu Mkuu Msaidizi wa Jumuiya hiyo Hossam Zaki amekiambia kituo cha televisheni cha al-Qahera kuwa mkutano huo utafanyika kwa njia ya video. Nayo tovuti ya habari ya taifa nchini Misri al-Ahram imeripoti kuwa mkutano huo umeitishwa kutokana na ombi lililotolewa na Saudi Arabia.

Mashambulizi ya kulipiza kisasi yaendelea kushuhudiwa Ghuba

Iran imefanya mashambulizi ya kulipiza kisasi katika baaadhi ya nchi za Mashariki ya Kati tangu Marekani na Israel zilipofanya mashambulizi ndani ya ardhi yake. Mashambulizi ya Iran yamekuwa yakizilenga kambi za kijeshi za Marekani na sehemu nyingine zikiwemo viwanja vya ndege.