1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

BAGHDAD: Irak yajadili kitisho cha Uturuki

16 Oktoba 2007
https://p.dw.com/p/C7FQ

Waziri Mkuu wa Irak,Nuri al-Maliki ameitisha mkutano wa dharura wa baraza lake la mawaziri kujadili vitisho vya Uturuki inayotaka kupeleka majeshi yake kaskazini mwa Iraq.Siku ya Jumatano,bunge la Uturuki litapiga kura ikiwa liidhinishe mswada wa serikali unaoshauri kupeleka majeshi yake kaskazini mwa Irak,kuwapiga waasi wa Kikurd wa PKK,walio na vituo vyao kaskazini mwa Irak.

Serikali za Irak na Marekani zimetoa mwito kwa Uturuki kutochukua hatua hiyo,zikiwa na hofu kuwa mashambulizi ya aina hiyo huenda yakavuruga hali ya utulivu katika eneo hilo la mpakani.