1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Urusi na Ukraine kurefusha makubaliano ya nafaka

Sudi Mnette
12 Machi 2023

Uturuki imeonesha imani kwamba mataifa ya Ukraine na Urusi yatakubaliana katika urefushaji wa mkataba wa kusafirisha nafaka inayokwamishwa na vita kupitia Bahari Nyeusi.

https://p.dw.com/p/4OZMS
Hafen von Odessa in der Ukraine
Picha: Metin Aktas/AA/picture alliance

Uturuki imeonesha imani kwamba mataifa ya Ukraine na Urusi yatakubaliana katika urefushaji wa mkataba wa kusafirisha nafaka inayokwamishwa na vita kupitia Bahari Nyeusi.

Waziri wa Ulinzi wa Uturuki Hulusi Akar ameliambia shirika la habari la Anadolu kwamba Urusi na Ukraine zipo katika muelekeo wa mtazamo wenye tija na kwamba wana imani hali hiyo itatoa matokeo chanya

Urusi ilizizuia bandari zote za Ukraine baada ya uvamizi wake wa Februari 24. Lakini kwa jitihada za Umoja wa Mataifa, Uturuki, Ukraine kadhalika na Urusi kulifikiwa makubaliano Julai 2022, usafirishaji wa shehena za nafaka kutoka katika bandari tatu zilizopo katika eneo la Bahari Nyeusi uliruhusiwa.

Makubaliano ya sasa yanafikia mwisho wake tarehe 18 Machi.