1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Imetimia miaka 36 tangu kuangushwa ukuta wa Berlin

9 Novemba 2025

Ujerumani inaadhimisha miaka 36 tangu kuanguka kwa Ukuta wa Berlin. Tukio hilo lilihitimisha enzi ya utengano na kufungua njia ya kuungana tena kwa iliyokuwa Ujerumani Magharibi na Mashariki.

https://p.dw.com/p/53L0Q
Ukuta wa Berlin ulitenganisha pande mbili za mji wa Berlin kati ya Ujerumani Magharibi na Mashariki.
Ukuta wa Berlin uliokuwa ukitenganisha Ujerumani Magharibi na Mashariki.Picha: Staff Sergeant F. Lee Cockran/Looks Film

Rais Frank-Walter Steinmeier atakuwa mwenyeji wa hafla ya kukumbuka siku hiyo pamoja na ghasia za mwaka 1938 dhidi ya Wayahudi. Steinmeier anatazamiwa pia kutoa hotuba katika makazi yake mjini Berlin itakayojikita katika kuimarisha demokrasia.

Kumbukumbu ya maumivu na chuki dhidi ya Wayahudi

Ofisi yake imesema kuwa Novemba 9 inaakisi kuibuka kwa mwangaza wa uhuru na demokrasia, pamoja na kumbukumbu ya maumivu na chuki dhidi ya Wayahudi.

Ukuta wa Berlin uliangushwa Novemba 9 mwaka 1989 na siku hiyo inaadhimishwa Ujerumani kama mwisho wa udikteta wa iliyokuwa Ujerumani Mashariki na kushindwa na itikadi ya kikomunisti ya Dola ya Kisovieti.