Qatar yahimiza kumalizika kwa mgogoro wa Marekani na Israel
21 Aprili 2026
Msemaji wa wizara ya mambo ya nje wa nchi hiyo Majed al-Ansari amesema vita hivyo vimeiweka kanda nzima, uchumi wa dunia na masoko ya nishati hatarini.
Al Ansari alijizuwia kuzungumzia kule kulikoitwa kufeli kwa mazungumzo ya Pakistan akisema dunia nzima inaunga mkono juhudi za Islamabad.
Ameongeza kuwa Qatar bado ina matumaini na inapendekeza angalau kurefushwa kwa muda wa usitishwaji mapigano iwapo makubaliano ya haraka hajatopatikana hadi.
"Ikiwa makubaliano hayakufikiwa, Qatar inaunga mkono hali ya sasa ya usitishaji vita, na tunategemea kuona muendelezo wa usitishwaji vita huo, hadi pale patakapopatikana suluhisho la kidiplomasia. Hapatamfaidi yoyote iwapo tutarejea katika uhasama."
Siku ya Jumapili Rais wa Marekani Donald Trump alisema ametuma ujumbe wake Pakistan, kuhudhuria mazungumzo hayo ambayo hadi sasa hayana uhakika wa kufanyika. Iran bado haijatuma wajumbe wake huko.