1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Iran na Marekani zatunishiana misuli, mazungumzo mashakani

21 Aprili 2026

Iran na Marekani zimetoleana kauli za vitisho wakati haijafahamika wazi ikiwa duru ya pili ya mazungumzo ya amani huko Islamabad itafanyika.

https://p.dw.com/p/5CYcy
Tehran I Spika wa Bunge la Iran Mohammad Bagher Khalibaf
Spika wa Bunge la Iran Mohammad Bagher Khalibaf akiwa mjini TehranPicha: Iranian Parliament Speaker Office/Handout/Anadolu Agency/IMAGO

Pakistan inaendelea na maandalizi ya mkutano huo, huku taarifa zikieleza kuwa Makamu wa rais wa Marekani JD Vance atasafiri siku ya Jumanne kuelekea Islamabad kuhudhuria mazungumzo hayo ikiwa yatafanyika. 

Rais wa Marekani Donald Trump ametishia kuishambulia vikali Iran ikiwa haitafikia  makubaliano mapya , huku Spika wa Bunge la Iran Mohammad Bagher Khalibaf akitaja kuwa wamejiandaa vilivyo na wako tayari kuonesha "mbinu mpya" kwenye uwanja wa vita.

Hayo yanajiri wakati makubaliano ya kusitisha mapigano kwa muda wa wiki mbili yaliyoanza kutekelezwa Aprili 8, yanatarajiwa kufikia tamati usiku wa leo, hali inayozusha hofu ya kuzuka tena kwa vita hivyo vya Mashariki ya Kati.