CDU yatabiriwa ushindi uchaguzi wa jimbo kubwa Ujerumani
15 Septemba 2025
Matangazo
Matokeo ya awali yanaonesha chama hicho cha Kansela Friedrich Merz kitajikingia hadi asilimia 33.7 ya kura kikifuatiwa na chama cha Social Democratic Party (SPD) kitakachopata asilimia 22.1 ya kura.
Chama cha mrengo mkali wa kulia cha AfD kitaambulia asilimia 15 pekee ambayo hata hivyo ni ongezeko la asilimia 5 ikilinganishwa na uchaguzi wa mwaka 2020.
Vyama vingine ikiwemo kile cha kijani (Die Grünne) na FDP vimepata matokeo mabaya. Uchaguzi kwenye jimbo hilo lenye wakaazi wengi zaidi nchini Ujerumani unazingatiwa kuwa kipimo cha umashuhuri binafsi na wa chama cha Kansela Merz aliyeingia madarakani mwezi Mei mwaka huu.