1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Ujerumani yataka kiti katika baraza la usalama la UN

28 Aprili 2026

Waziri wa mambo ya nje Johann Wadephul,yuko Newyork kutafuta uungaji mkono nchi yake kupata kiti kisicho cha kudumu katika baraza la usalama la UN

https://p.dw.com/p/5Cwoo
Johann Wadephul waziri wa mambo ya nje wa Ujerumani akishiriki katika kikao cha baraza la usalama la  Umoja wa Mataifa
Johann Wadephul waziri wa mambo ya nje wa Ujerumani akishiriki katika kikao cha baraza la usalama la Umoja wa MataifaPicha: Lev Radin/Sipa USA/picture alliance

Waziri wa mambo ya nje wa Ujerumani Johann Wadephul anatarajiwa hivi leo, kuimarisha kampeini ya nchi yake ya kutaka kupatiwa kiti kisicho cha kudumu katika baraza la usalama la Umoja wa Mataifa kabla ya mchakato wa  kura kwenye baraza kuu la Umoja huo Juni 3.

Wadephul atakutana na mabalozi kutoka nchi wanachama wa Umoja wa Mataifa mjini New York kuipigia debe nchi yake kupata kiti hicho kwa mwaka 2027 hadi 2028.

Katika juhudi zake hizo,waziri huyo wa mambo ya nje wa Ujerumani pia atawasilisha nia ya Ujerumani kwa wajumbe kutoka mataifa 54 ya bara la  Afrika , kundi ambalo ni muhimu katika kura hiyo.

Somalia,Jamhuri ya kidemokrasia ya Kongo na Liberia zinashikilia kwa sasa viti visivyo vya kudumu katika baraza la usalama la Umoja wa Mataifa.

Ujerumani imekuwa ikiunga mkono wito wa mataifa ya Afrika wa kudai mageuzi kwenye baraza la usalama la Umoja wa Mataifa, ikiwa ni pamoja na bara hilo kutaka alau viti viwili vya kudumu na kura ya turufu.