1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
SiasaAfghanistan

Taliban yasaini makubaliano ya dola bilioni 6.5 Afghanistan

Sylvia Mwehozi
1 Septemba 2023

Serikali ya Taliban inayotawala nchini Afghanistan imesaini mikataba saba yenye thamani ya takribani dola bilioni 6.5 ya uwekezaji.

https://p.dw.com/p/4Vr9D
Ghasni Afghanistan
Picha: Hector Retamal/AFP

Makubaliano haya ni makubwa zaidi tangu  Taliban iliporejea mamlakani miaka miwili iliyopita.

Mikataba hiyo imetiwa saini kati ya serikali na makampuni ya ndani ambayo mengi yana ushirika na makampuni kigeni kutoka China, Iran na Uturuki. Aidha mikataba hiyo inahusiana na shughuli za kufua chuma, uchimbaji wa madini ya risasi,  zinki na dhahabu katika majimbo manne.

Makubaliano hayo yanatajwa kuwa yatasaidia kuupatikana maelfu ya nafasi za kazi  na kuimarisha kwa kiasi kikubwa hali ya uchumi nchini Afghanistan. Hata hivyo hakukuwa na taarifa yoyote kuhusiana na makubaliano hayo kutoka wizara ya Madini na Petroli.