1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Magazetini

Abdu Said Mtullya9 Septemba 2009

Katika maoni yao wahariri wa magazeti ya Ujerumani leo wanazungumzia juu ya Afghanistan.

https://p.dw.com/p/JYhu
Mpiga kura katika uchaguzi wa nchini Afghanistan.Picha: AP

Wahariri wa magazeti ya Ujerumani leo wanazungumzia juu ya  uchaguzi wa rais nchini  Afghanistan, tamko la kansela Angela Merkel  juu  ya shambulio  lililofanywa na ndege  za  Marekani kwa niaba  ya kikosi  cha Ujerumani nchini   Afghanistan.

Wahariri  hao  pia wameandika  juu  ya  ripoti ya  kiwango  cha elimu nchini  Ujerumani iliyotolewa  na shirika la ushirikiano  wa uchumi na maendeleo  OECD.

Juu  ya uchaguzi wa  rais  nchini Afghanistan  gazeti la Financial Times Deutschland  linasema  yeyote  anaetaka kuleta demokrasia nchini Afghanistan kwa kutumia vigezo vya magharibi atakuwa  sawa na mtu  anaenunua  punda kiwete.!   Sababu ni kwamba  katika mazingira  ya   Aghanistan demokrasia ni msingi  tu wa kujaribu  kuleta utulivu nchini.

Gazeti la  Financial Times  Deutschland linaeleza kwamba  uhalali  wa  serikali  ya rais Karzai umetiwa dosari  na madai juu ya udanganyifu uliofanyika katika  kuhesabu kura. Na ndiyo sababu,ni lazima  kura zihesabiwe tena katika maeneo  ambako madai hayo yametolewa.

Wahariri  wa  magazeti pia wametoa maoni yao juu ya shambulio lililofanywa na ndege za Marekani baada  ya  kamanda wa majeshi  ya Ujerumani  kuomba msaada.

Katika shambulio hilo, katika jimbo la Kunduz raia  zaidi ya 130  waliuawa. Jeshi la Ujerumani  limelaumiwa  vikali ndani na  nje kwa vifo vya  rais  hao. Lakini Kansela     wa Ujerumani  Angela Merkel alitetea  uamuzi wa kamanda  wa jeshi la Ujerumani katika tamko alilotoa bungeni jana.  Gazeti la Neue Osnabrücker  linasema katika maoni yake kwamba msimamo  wa Kansela Merkel ni sahihi kabisa katika kupinga  lawama zinazotoka  nje na ndani juu ya  shambulio hilo lililoelekezwa dhidi ya  taliban.

Mhariri wa Neue Osnabrücker anatilia maanani kwamba Kansela Merkel  hakurudi nyuma  bungeni katika msimamo   wake,  juu ya Afghanistan  na  badala yake amewataka wananchi wa  Ujerumani  watambue umuhimu wa  jukumu la jeshi la Ujerumani nchini Afghanistan.Mhariri huyo anasema wajerumani wanahitaji kuwa na moyo  wa kuwa  tayari kujitoa mhanga na kusonga mbele.

Lakini mhariri wa  Reutlinger General Anzeiger hakubaliani na hayo. Mhariri  huyo anasema,  ni kweli  kwamba Kansela Merkel amezungumza vizuri bungeni, lakini lingekuwa  jambo zuri zaidi iwapo serikali yake  ingefanikiwa  katika  ujenzi  wa Afghanistan na kuondoka haraka.

Shirika la ushirikiano wa uchumi na maendeleo OECD limetoa ripoti juu ya elimu katika nchi  za shirika hilo.Ripoti hiyo imeonyesha kuwa Ujerumani  inalega nyuma ya nchi nyingi. Juu ya hayo gazeti la Oldenburgische Volkszeitung linasema

"Wanasiasaa nchini Ujerumani  wanafikiria tu juu ya ustawi  wa uchumi, takwimu za bajeti na  asilimia  za kodi." Gazeti linasema hayo ni sawa,lakini bila  ya kuekeza katika maendeleo ya elimu na utafiti  hapatakuwa na ustawi. Kwa hiyo viongozi  wanatakiwa halakuli  hali,wachukue hatua thabiti.

Mwandishi/Mtullya /Deutsche Zeitungen

Mhariri/ Abdul-Rahman

.....