Ulaya yatakiwa kuongeza nguvu zaidi kwenye ulinzi
28 Januari 2026
Matangazo
Kallas Ameyasema hayo katika mkutano wa ulinzi unaofanyika mjini Brussells. Ameeleza kuwa Ulaya inapaswa kukubaliana na uhalisia mpya kwani siyo tena eneo kuu linalotegemewa na Washington.
Kitisho cha kuinyakua Greenland ni tahadhari kwa Ulaya
Mkuu huyo wa Sera za Kigeni wa Umoja wa Ulaya ametoa kauli hiyo wiki kadhaa baada ya Trump kutishia kuinyakua Greenland kutoka kwa Jumuiya ya Kujihami ya NATO na kutoka kwa Denmark ambayo ni mwanachama wa Umoja wa Ulaya.
Nchi za umoja huo zimeshaongeza bajeti zao za Ulinzi tangu Urusi ilipoivamia Ukraine. Zilikubaliana pia kuongeza bajeti ya ulinzi katika Jumuiya ya NATO kutokana na shinikizo la Trump.