1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

FREETOWN: Hali ya wasiwasi yatanda huku matokeo ya uchaguzi yakisubiriwa

14 Agosti 2007
https://p.dw.com/p/CBZH

Polisi nchini Sierra Leone iko katika hali ya tahadhari kabla matokeo ya mwisho ya uchaguzi kutolewa.

Hali ya wasiwasi imetanda nchini humo baada ya matokeo ya awali kuonyesha kuwa chama cha upinzani cha All People´s Congress, APC, kinaongoza na upinzani umewatolea mwito wafuasi wake wajitokeze barabarani kusherehekea ushindi.

Rais Ahmad Tejan Kabbah ameviamuru vikosi vya usalama viwe katika hali ya tahadhari ili kukabiliana na machafuko yoyote yatakayotokea.