Ahmedinejad asema ripoti ya upelelezi ni ushindi kwa Iran
5 Desemba 2007Matangazo
Rais wa Marekani George W.Bush ameuambia mkutano wa waandishi wa habari mjini Washington kuwa Iran bado ni tishio kwa amani duniani.Siku ya Jumatatu ripoti mpya ya upelelezi iliyotolewa na idara 16 za Marekani kuhusu Iran ilisema,Tehran ilisitisha juhudi za kutengeneza silaha za atomu katika mwaka 2003.
Kwa upande mwingine Rais wa Iran Mahmoud Ahmedinejad amesema,ripoti hiyo ni tangazo la ushindi kwa mradi wa nyuklia wa Iran.Lakini Waziri Mkuu wa Israel Ehud Olmert akishukia ripoti hiyo amekariri kuwa Israel itaendelea kujitahidi kuizuia Iran kujipatia silaha za nyuklia.