1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

UN yalaani vurugu zinazoshuhudiwa Mashariki ya Kati

28 Februari 2026

Mkuu wa haki za binaadamu wa Umoja wa Mataifa Volker Turk amelaani vurugu zinazoshuhudiwa Mashariki ya Kati na kuzitaka pande zote kurejea kwenye mazungumzo, na kuwa mashambulizi yatasababisha vifo, uharibifu na mateso.

https://p.dw.com/p/59aRX
Geneva I Mkuu wa haki za binaadamu wa Umoja wa Mataifa Volker Turk
Mkuu wa haki za binaadamu wa Umoja wa Mataifa Volker Turk akihutubia mjini GenevaPicha: Kyodo News/IMAGO

Aidha Turk amesema viongozi mbalimbali wamekuwa wakitumia madaraka vibaya na kutoa kipaumbele kwa matumizi ya nguvu kutatua mizozo, hali inayopelekea kuongezeka kwa idadi ya mizozo kote duniani.

Turk amesema idadi ya migogoro inayohusisha silaha imeongezeka maradufu tangu mwaka 2010 na kufikia karibu migogoro 60, huku akitamatisha kuwa kwa sasa dunia inazidi kuwa eneo hatari zaidi.

Aidha,  Umoja wa Afrika na mataifa mengine kama Ujerumani, Ufaransa, Uingereza, Brazil na mengineyo yametoa wito wa kusitisha mashambulizi huko Mashariki ya Kati na kurejea kwenye mazungumzo.