Ulaya yahimiza suluhu ya kidiplomasia mzozo wa Iran
23 Februari 2026
Mkuu wa sera za nje wa Umoja wa Ulaya Kaja Kallas ametowa wito wa kuzingatiwa suluhu ya kidiplomasia kuhusu Iran, kabla ya kuanza tena kwa mazungumzo mengine kati ya Iran na Marekani wiki hii.
Wito huo umetolewa chini ya kiwingu cha vitisho vilivyotolewa na rais Donald Trump dhidi ya Tehran.Iran yasema huenda ikakutana na Marekani jijini Geneva Alhamisi
Mwanadiplomasia huyo wa ngazi za juu katika Umoja wa Ulaya amesisitiza kabla ya kuanza kwa mkutano wa mawaziri wa mambo ya nje wa Jumuiya hiyo, kwamba Ulaya ina mambo mengi na haitaki kuona vita vingine.
Jana waziri wa mambo ya nje wa Iran Abbas Aragchi alisema kwamba ufafanuzi wa kile kinachoweza kuwa mpango wa makubaliano, unaandaliwa kabla ya mazungumzo yatakayofanyika siku ya Alkhamisi, chini ya usimamizi wa Oman.