1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Ujumbe wa Pakistan uko Tehran ukitarajia mazungumzo

16 Aprili 2026

Mkuu wa jeshi wa Pakistan Asim Munir amekutana na waziri wa mambo ya kigeni wa Iran Abbas Araghchi huko Tehran.

https://p.dw.com/p/5CFpj
Waziri Mkuu wa Pakistan Shehbaz Sharif
Waziri Mkuu wa Pakistan Shehbaz SharifPicha: Pakistan's Prime Minister Office/AFP

Hii ni katika hatua ya hivi karibuni ya kupunguza mivutano huko Mashariki ya Kati na kupanga awamu ya pili ya mazungumzo kati ya Marekani na Iran baada ya karibu wiki saba za vita.

Pakistan imeibuka kama mpatanishi muhimu baada ya kuwa mwenyeji wa mazungumzo kati ya Marekani na Iran mjini Islamabad.

Mamlaka zinasema mazungumzo hayo yalisaidia kupunguza tofauti zilizoko kati ya mataifa hayo mawili yaliyo kwenye mzozo.

Na sasa wapatanishi wanatafuta kufanyika awamu nyengine ya mazungumzo kabla muda wa mwisho kufika wiki ijayo.

Ikulu ya White House imesema awamu nyengine ya mazungumzo huenda ikafanyika nchini Pakistan ingawa hakuna uamuzi uliofanyika kufikia sasa iwapo kufanyike mazungumzo kwa mara nyengine.

Licha ya vizuizi hivyo vya Marekani katika bandari za Iran, maafisa wa kikanda wanaripoti kuwa hatua zinapigwa huku maafisa ambao hawakutaka kutambulishwa wakisema, Marekani na Iran wana "makubaliano ya msingi" ya kuongeza usitishwaji mapigano ili kutoa fursa zaidi ya diplomasia.