Tuzo ya amani ya Westfalia
11 Oktoba 2008Matangazo
MÜNSTER:
Katibu mkuu wa zamani wa Umoja wa mataifa Kofi Annan ametunukiwa zawadi ya amani ya Westfalia.Licha ya misuko suko yote iliyotokea,Kofi Annan ameendelea kuamini amani inaweza kupatikana ulimwenguni" wamesema hayo wasimamizi wa tuzo hiyo mjini Münster.Zawadi hiyo yenye thamani ya yuro 50 elfu hutolewa kila baada ya miaka miwili.Tuzo ya amani ya Westfalia imeanza kutolewa tangu mwaka 1998.