Trump asema mwafaka kuhusu Greenland umefikiwa
22 Januari 2026
Matangazo
Trump ameyasema hayo wakati ambapo pia amedai kuwa hatotumia nguvu kukichukua kisiwa cha Greenland na pia kudai kuwa hatoziwekea tena ushuru bidhaa za mataifa nane ya Ulaya yaliyokuwa yanaupinga mpango wake wa kuitwaa Greenland.
Akizungumza na kituo cha habari cha Marekani CNBC, Trump amesema makubaliano hayo ni ya muda mrefu na kila mmoja ameyafurahia ila hakutoa taarifa zaidi na hakusema pia iwapo hiyo inamaanisha kuwa Marekani itakuwa na udhibiti wa kisiwa hicho cha eneo la Arctic.
Trump ameyasema yote hayo baada ya mkutano huko Davos na Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Kujihami ya NATO Mark Rutte ambaye kupitia msemaji wake, ameyathibitisha hayo aliyoyasema Trump.