1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Timu ya Togo yarejea nyumbani

11 Januari 2010

Timu ya taifa ya kandanda ya Togo imerejea nyumbani, kutoka Angola ilikojitoa katika michuano ya Afrika kufuatia shambulio dhidi yao lililofanywa na waasi katika mji wa Cabinda.

https://p.dw.com/p/LQDL
Timu ya taifa ya TogoPicha: AP

Timu hiyo imerejea ikiwa na miili ya kocha msaidizi  na afisa habari wa michezo ambao pamoja dereva wa basi lao waliuawa katika shambulio hilo hapo siku ya Ijumaa.

Waziri Mkuu wa Togo Gilbert Fossoun Houngbo alitangaza kujitoa kwa nchi hiyo ingawaje wachezaji walitaka kuendelea na mashindano.

Naye Waziri wa michezo wa Togo Christophe Tchao akizungumz na waandishi wa habari kabla ya kupanda ndege iliyotumwa na serikali yao, alisema kuwa ameliomba shirikisho la soka barani Afrika CAF kuangalia uwezekano wa kuiweka tena nchi hiyo katika ratiba ya michuano hiyo baada ya siku tatu za maombolezi.

Mwandishi:Aboubakary Liongo

Mhariri:Thelma Mwadzaya