Rwanda yapiga marufuku adhabu ya kifo
28 Julai 2007Matangazo
Kamishna wa Baraza la Haki za Binadamu la Umoja wa Mataifa,Bibi Louise Arbour amesema,hatua hiyo inafungua njia ya kuwafikisha mahakamani washukiwa mauaji ya halaiki nchini Rwanda,ambako kiasi ya watu 800,000 waliuawa katika mwaka 1994.
Shirika la Amnesty International limesema,Rwanda imekuwa nchi ya kwanza katika kanda ya Maziwa Makuu,kupiga marufuku adhabu ya kifo na kuthibitisha mwenendo wa dunia nzima,kukomesha adhabu ya kifo.