Marekani kuipima Urusi kama ina nia ya kumaliza vita Ukraine
14 Februari 2026
Matangazo
Marekani imesema inabidi ipime na kuangalia kwanza iwapo kweli Urusi inataka kusitisha vita vyake huko.
Akizungumza katika mkutano wa usalama unaofanyika Munich Ujerumani, Rubio amesema hawana hakika iwapo Urusi ina nia ya kweli ya kusitisha vita hivyo, lakini Marekani itaendelea kuishinikiza ili kukomesha vita hivyo vitakavyoingia mwaka wake wa tano hivi karibuni.
Huku hayo yakiarifiwa nchini Ukraine kwenyewe shambulizi la Urusi lililotokea usiku wa kuamkia leo mjini Odesa lililenga jesngo la wakaazi na kusababisha kifo cha mwanamke mmoja, hii ikiwa ni kulingana na gavana wa eneo hilo la Kusini mwa Ukraine.