SiasaAfrika Kusini
Raia watano wa Msumbiji wauawa Afrika Kusini
3 Juni 2026
Matangazo
Maandamano dhidi ya wageni wasiokuwa na vibali yamekuwa yakiongezeka katika wiki za hivi karibuni.
Ghana imewahamisha raia wake 300, na Nigeria imetangaza kuchukuwa hatua kama hiyo.
Ghasia zilizuka kwenye mji wa pwani wa Mossel Bay siku ya Ijumaa, ambapo waandamanaji walichoma moto maduka ya raia wa kigeni, wengi wao kutokea mataifa ya Afrika.
Katika taarifa yake ya siku ya Jumatatu, serikali ya Msumbiji ilisema raia wake saba wamefariki dunia nchini Afrika Kusini, watano kati yao wakiwa wameshambuliwa na waandamanaji. Jeshi la polisi limethibitisha vifo viwili tu kati ya hivyo.
Haya ni mauaji ya kwanza kwenye wimbi la sasa la ghasia zinazochochewa na chuki dhidi wa wageni.