1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
Migogoro

NATO kujadili udhibiti wa nyuklia na utengezaji wa silaha

15 Juni 2023

Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Kujihami-NATO Jenerali Jens Stoltenberg amesema mataifa ya muungano huo yatajadili namna ya kudhibiti nyuklia.

https://p.dw.com/p/4SaeE
NATO Katibu mkuu Jens Stoltenberg akiwa Washington
Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Kujihami-NATO Jenerali Jens Stoltenberg Picha: Jonathan Ernst/REUTERS

Brussels 

Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Kujihami-NATO Jenerali Jens Stoltenberg amesema mataifa ya muungano huo yatajadili namna ya kudhibiti nyuklia na mipango ya kuhifadhi silaha katika mikutano ijayo ya  mawaziri wa ulinzi wa mataifa ya jumuiya hiyo.

Amesema kadhalika mawaziri hao wanapanga kujadili kupanua uwezo wa uzalishaji kwa silaha muhimu, jambo ambalo litatolewa uamuzi katika mkutano wa kilele wa NATO wa mwezi ujao.

NATO: Ukraine inapiga hatua katika uwanja wa mapambano

Mkutano wa mawaziri wa ulinzi wa NATO unatarajiwa kuanza leo hii Alhamisi kwa mazungumzo na wawakilishi kutoka sekta ya utengenezaji wa silaha na kamisheni ya NATO kwa Ukraine. Mada kuu ni vita inayoendelea ya Urusi dhidi ya Ukraine na matokeo yake.