Mvutano bomba la mafuta la Druzhba wazidi makali
6 Machi 2026
Matangazo
Waziri Mkuu wa Hungary Victor Orban amekiambia kituo cha redio ya taifa leo Ijumaa, kuwa serikali mjini Budapest imekwishazuia upelekaji mafuta ya diesel nchini Ukraine na kwamba imedhamiria kuzuia bidhaa zote kupelekwa nchini humo mpaka bomba la mafuta la Druzhba litakapoanza tena kufanya kazi.
Kusimama kwa usafirishaji mafuta kupitia bomba la Druzhba kumekuwa chanzo cha mvutano mkubwa kati ya Ukraine na Hungary pamoja na Slovakia.
Ukraine imesema limeharibiwa na mashambulizi ya Urusi na inafanya jitihada zote kulikarabati. Hata hivyo, Hungary na Slovakia zimeishutumu Ukraine kufanya kazi hiyo kwa kasi ya kujikokota.