1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Marekani yatoa waranti kukamatwa kwa meli ya mafuta ya Iran

Sekione Kitojo
17 Agosti 2019

Wizara ya  sheria  ya  marekani imetoa waranti jana Ijumaa (16.08.2019) ya kukamatwa kwa  meli ya  mafuta  ya  Iran Grace 1, siku moja  baada  ya  jaji  wa  Gibraltar kuruhusu kuachiliwa kwa meli hiyo iliyokamatwa.

https://p.dw.com/p/3O37r
Supertanker «Grace 1» liegt vor Gibraltar
Picha: picture-alliance/dpa/AP/M. Moreno

 

Wizara ya sheria  inadai kuwa  meli  hiyo ni  sehemu  ya  mpango "wa kufikia  kinyume  na  sheria mfumo wa  kifedha  wa  Marekani, kusaidia  upelekaji  kinyume  na  sheria mafuta  nchini  Syria  kutoka Iran unaofanywa  na  jeshi  la kulinda  mapinduzi  ya  Kiislamu," ambayo  Marekani  imesema  kuwa  ni  kundi  la  kigeni  la  kigaidi.

Supertanker «Grace 1» liegt vor Gibraltar
Meli ya mafuta ya Iran Grace 1 ikiwa katika eneo la GibraltarPicha: AFP/J. Guerrero

waranti  huo unasema  meli  hiyo, ambayo  bado  imetia  nanga katika  eneo  hilo linalo milikiwa  na  Uingereza la Gibraltar hadi  jana Ijumaa, na  mafuta  yote  yaliyomo  katika  meli  hiyo  yanalazimika kutaifishwa  kwa  misingi ya  ukiukaji wa  sheria  ya  kimataifa  ya nguvu  za  dharura  za  kiuchumi , pamoja  na  kukamatwa kwa  kiasi cha  dola  995,000 , katika  akaunti ambayo  haikutajwa  katika benki  moja  nchini  Marekani  inayoshrikiana  na  kampuni  ya biashara  ya  Paradise Global Trading LLC, ambayo  imeiita kampuni  ya  Shell inayohusishwa  na  biashara  ambayo inafanyakazi  kwa  niaba  ya  jeshi  la  Iran.

Hakuna taarifa za  haraka  kutoka  Uingereza  ama  Gibraltar kuhusiana  na  iwapo  watachukua  hatua  kuhusiana  na  waranti huo, wakati  Iran  imesema  inatuma  wafanyakazi  wengine  wapya kuiendesha  meli  hiyo  pamoja  na  shehena  yake xa  mapipa milioni 2.1 ya  mafuta.

Öltanker auf dem Weg nach Syrien in Gibraltar festgesetzt
Meli ya jeshi la majini la Uingereza ikiwa katika doria katika eneo la GibraltarPicha: Reuters/J. Nazca

Jaji akataa  ombi  la  Marekani

Jaji  alikataa  hatua  ya  dakika  za  mwisho  ya  kisheria  kutoka marekani ikidai  kuwa  meli  hiyo ibakie  imekamatwa. Kukamatwa kwa  meli  hiyo  Julai 4  kumekuja  huku  kukiwa  na  hali  ya  wasi wasi  mkubwa  katika  eneo  la  ghuba  baada  ya  mashambulizi kadhaa  yanayodaiwa  kufanywa  na  Iran  katika  meli  ndogo  za mafuta.

Marekani ikieleza  kuhusu kitisho  cha  Iran kwa  washirika  wa Marekani, ilipanua  uwezo wake  wa  kijeshi  katika  eneo  hilo kwa kupeleka  meli  mpya za  kubebea  silaha  na  ndege , makombora pamoja  na  ndege za  ushambuliaji za  mkakati.

Iran na  Marekani zimekuwa zikivutana  tangu  pale  rais wa Marekani Donald Trump alipoitoa  nchi  hiyo  katika  makubaliano muhimu  ya  kinyuklia  mwaka  2015 baina  ya  mataifa  makubwa yenye  nguvu  na  Iran , na  kurejesha  vikwazo ambavyo  vinaathari kubwa  katika  uchumi wa  Iran.

Öltanker Stena Impero liegt nun vor dem Hafen von Bandar Abbas
Meli ya mafuta inayopeperusha bendera ya Uingereza Stena Impero iliyokamatwa na IranPicha: AFP/N. Kemps

Baada  ya  kukamatwa  kwa  meli  ya  Grace 1, Julai 19 Iran ilikamata  meli  yenye  bendera  ya  Uingereza  ya  mafuta  Stena Impero  katika  ujia  wa  bahari  wa  Hormuz.

Iran inasema  meli  hiyo ilikiuka "sheria  za  kimataifa  za  safari za baharini,"  lakini  hatua  hiyo inaonekana  kwa  kiasi kikubwa  kuwa ni  kulipiza  kisasi kwa  kukamatwa  kwa  Grace 1.