1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Uamuzi wa chama cha SPD.

Mtullya, Abdu Said27 Mei 2008

Chama cha SPD chamteua profesa Gesine Schwan kugombea urais wa Ujerumani.

https://p.dw.com/p/E6wy
Profesa Gesine Schwan-mjumbe wa chama cha SPD katika uchaguzi wa rais nchini Ujerumani.Picha: DW

Katika  maoni  yao  wahariri  wa  magazeti karibu yote ya Ujerumani leo wanazungumzia  juu ya uamuzi wa  chama cha Social Demokratik  SPD  kumteua mjumbe wake kugombea wadhifa  wa  rais nchini Ujerumani.

Gazeti la Hannoversche Allgemeine pia linazungumzia  juu ya uamuzi wa  chama cha  social  demokratik SPD  ambacho pia kimo  katika  serikali  ya mseto,  wa kumteua   mjumbe wake  prof. Gesine Schwan  kugombea wadhifa wa rais, na hivyo  kupambana  na rais wa  sasa  Horst Köhler -mwanachama  wa chama  cha CDU  kinachoongoza  serikali  ya  mseto ya Ujerumani

Rais huyo  wa sasa  anawania kipindi  cha pili.

Gazeti la Hannoversche  Allgemeine linasema chama cha  SPD kimecheza mchezo wa  patapotea kwa  kupitisha uamuzi  huo.

Mhariri wa gazeti hilo anasema wasiwasi uloikuwapo ni kwamba  huenda  chama hicho mwishowe kikafutu  msimamao   wa wananchi. Gazeti linatamka kuwa idadi kubwa ya wananchi wa Ujerumani wanataka rais  wa  sasa  Horst  Köhler  aendelee na kipindi cha  pili. Sababu ni   kwamba hadi sasa Horst Köhler   ameiwakilisha Ujerumani  vizuri sana.

Gazeti la  Südkurie linatilia maanani   kuwa hii ni mara ya pili kwa mjumbe huyo wa SPD profesa Gesine Schwan kujaribu kuwania wadhifa  huo.

Hoja  iliyopo ni kwamba ikiwa chama  cha CDU kina Kansela  mwanamke  basi chama cha  SPD  nacho kinastahili  kuwa na mjumbe  wake  mwanamke  kama  rais wa chini. Lakini katika hayo  chama hicho kinakabiliwa na mtanziko  mkubwa.

Mjumbe wake hatawaweza  kumshinda rais wa sasa  bila  ya  msaada wa kura  za chama cha mlengo wa shoto.

Na hakika ni  vigumu sana kwa  mwenyekiti wa  chama  cha SPD bwana Kurt  Beck kuwaeleza  wapiga  kura juu ya uhusiano wa chama chake na chama  cha mlengo wa shoto, yaani wakomunisti wa  zamani.Na gazeti jingine, Braunschweig Zeitung linasema  chama cha SPD kinaweza kujaribu kuligeuza suala hilo, ndani nje,  au juu chini  lakini ukweli  utabaki  palepale Chama  hicho kimetoa  ishara ya  kuelekea mlengo wa  shoto.

Hatahivyo  mhariri  wa  gazeti la Saarbrücker anesema ni haki ya  chama  cha SPD kuwa na mjumbe  wake katika  uchaguzi wa rais.