1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
SiasaJapan

Japan, Korea Kusini na Marekani kuimarisha ushirikiano wao

17 Aprili 2024

Waziri Mkuu wa Japan Fumio Kishida amesema kuwa ameafikiana na rais wa Korea Kusini Yoon Suk Yeol kuimarisha ushirikiano kati ya Tokyo, Washington na Seoul.

https://p.dw.com/p/4etJZ
Rais wa Marekani Joe Biden na Waziri Mkuu wa Japan Fumio Kishida
Rais wa Marekani Joe Biden na Waziri Mkuu wa Japan Fumio KishidaPicha: Susan Walsh/AP/picture alliance

Kishida na Rais wa Marekani Joe Biden walifanya mazungumzo wiki iliyopita na kukubaliana, pamoja na mambo mengine, juu ya ushirikiano wa karibu wa mataifa matatu ya Japan, Marekani na Korea Kusini.

Hatua hii ni katika dhamira ya kukabiliana na kitisho kutopka kwa Korea Kaskazini ambayo imekuwa ikiendeleza mikakati yake ya silaha za nyuklia pamoja na makombora ya masafa marefu.