MigogoroUkraine
Watu wawili wauawa kwenye shambulio la droni Kherson
2 Mei 2026
Matangazo
Watu wawili, mwanaume na mwanamke, wameuawa na wengine saba wamejeruhiwa katika shambulio la droni la Urusi lililolenga basi dogo katika mji wa Kherson kusini mwa Ukraine. Gavana wa kijeshi wa eneo hilo, Oleksandr Prokudin, amesema waliojeruhiwa, wakiwemo wanaume sita na mwanamke mmoja, wamepelekwa hospitalini kwa matibabu.
Mji wa Kherson ulitekwa na majeshi ya Urusi mwanzoni mwa uvamizi mkubwa wa mwaka 2022, lakini baadaye walijiondoa kufuatia mashambulizi ya kujibu ya Ukraine.
Tangu wakati huo, eneo la mapigano limekuwa karibu na mji huo, ambao unaendelea kushambuliwa mara kwa mara kwa droni na makombora ya masafa marefu kutoka Urusi.