WASHINGTON: Mkutano juu ya kitisho cha ugaidi wa kinyuklia wiki ijayo nchini Morokko
28 Oktoba 2006Matangazo
Wajumbe kutoka nchi kiasi ya 10 watakutana mjini Rabat nchini Morokko kuzungumzia juhudi za kupambana na kile walichokitaja kitisho cha ugaidi wa kinyuklia: Wizara ya mambo ya kigeni ya Marekani inasema mkutano huo ni katika mpango ulioanzishwa na Marekani na Rushia mwezi Julai mwaka huu. Mkutano huo utawajumuisha wajumbe kutoka Marekani, Rushia, Ufaransa, Uingereza, Ujerumani, Italy, Japan, Canada, Uchina, Kazakhstan na Uturuki. Morokko, mwenyeji wa mkutano huo, inazingatiwa na Marekani pamoja na Rushia kuwa inachangia vya kutosha katika juhudi za kupambana na ugaidi duniani.